TAFUTA HAPA

HADITHI: Damu, mabusu na machozi SEHEMU YA 20

Hakusinzia mpaka asubuhi na kitu cha kwanza alichokifanya baada ya kuamka ni kwenda kwenye kibanda cha babu Ayoub kumwangalia mtoto wake, hapakuwa na mtu yeyote ndani ya kibanda! Alirudi haraka hadi ndani na kumuuliza mzee Kiwembe kama alikuwa na taarifa juu ya walikokuwa wameelekea.
“Labda wako ufukweni wanaoga?”
“Acha nikawaangalie!”
Alikimbia kwenda ufukweni, alikuwa na hamu ya kufahamu kama kuna madhara yoyote yaliyompata Nancy kutokana na kitendo alichofanyiwa usiku! Kabla hajafika ufukweni alikutana nao wakikimbizana, Nancy alikimbia akiwa uchi wa mnyama na kuimba nyimbo nyingi zisizoeleweka, akitaja na kuliita jina la Tonny kila baada ya maneno machache.
“Nancy!Nancy!Nancy!”Mama yake alimwita alipowafikia lakini mwanae hakumjali wala kumwitikia.
“TOKAAAA!TOKAAA MBELE YANGU MCHAWI MKUBWA WEEE!” Nancy alimwambia mama yake huku akimmwagia mchanga, maumivu yaliyompata mama Nancy moyoni mwake hayakuwa na maelezo! Machozi yalimiminika kama chemchem, lawama nyingi alizitupa kwa babu Ayoub.
“Mnaona sasa mlivyomfanya mwanangu, tulijitahidi kuwaelewesha juu ya kiapo alichokula lakini hamkutaka kuamini, tutafanya kitu gani sasa? Tayari ameshakuwa mwendawazimu!’
“Aa wapi! Hizi ni mbwembwe zake tu ili asishiriki tendo la ndoa, atake asitake huyu ni mke wangu lazima atafanya tu ! ” 
“Lakini umemsababishia matatizo mtoto wangu! ” 
“Hilo mimi sijali ! ” 
“Nguo zake ziko wapi? ”Aliuliza mama Nancy.
“Amezitupa sehemu fulani huko ufukweni alikokuwa akikimbia ovyo!”Sehemu gani? ” Sifahamu ! Amenisumbua sana na bila kumshika angekufa maji kwa sababu alikuwa anataka kudumbukia majini ili afe ! Nancy ! Nancy ! Nancy ! Mama alimwita binti yake, badala ya kuitika Nancy aliendelea kukimbia huku akicheka na kuongea maneno yasiyoeleweka, tayari alikuwa mwendawazimu ! Kiapo alichokula kwa mganga kilikuwa kimemdhuru. 
“Hahaaaa ! I don’t care ! I don’t mix milk and sugar ! I don’t go ! Here and there, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere is my hero. I love Saddam Hussein ! Haaaaa ! Haaaaa ! Haaaaa ! ” Nancy aliendelea kuongea mambo yasiyoeleweka na kuzidi kuumiza moyo wa mama yake aliyekuwa akilia huku akimfuata kwa nyuma . 
Kila alipomkaribia Nancy alizidi kukimbia kwenda mbele zaidi mpaka alipokamatwa na mzee Kiwembe na kubebwa juu hadi kwenye kibanda cha babu Ayubu 
“ Anajifanya mjanja ! Atatulia tu, hapa ni kisiwani bwana mambo ya hapa ni ya kijeshi-jeshi na ni lazima azae” Alijitapa babu Ayubu. 
Mama yake alisikitika mno na hakuelewa ni kwa namna gani angeweza kuondoka kisiwani na mtu ambaye hakutaka hata kumkaribia, mipango yote ya kutoroka aliyoiongea na Nancy kabla hajapatwa na wendawazimu ilionekana kuwa migumu, kulikuwa na dalili kwamba maisha yao yangekuwa hapo kisiwani siku zote kama asingepatikana mtu wa kuwaokoa.
“ Na huyo mtu ataambiwa na nani kwamba tuko hapa ? Na sijui hivi sasa mzee Katobe anafikiria nini kuhusu mimi, nafikiri haelewi matatizo yanayonipata ! Nitakufa hapa bila kumwona” Aliwaza mama Nancy akimwangalia mwanae akifungwa miguu na mikono na kuunganishwa kwenye nguzo iliyokuwa katikati ya kibanda.

****
Hayo ndiyo yakawa maisha yao, Nancy akawa ni mtu wa kukaa kwenye kamba mchana na usiku, pamoja na kuwa mwehu hakuipenda hali hiyo, mara kwa mara alijaribu kujiondoa kwenye kamba lakini alishindwa. 
Nyama za mikono na miguu yake zililiwa na kamba zilizomkaza na kumsababishia vidonda ! Mama yake alijitahidi kumwosha kila siku lakini alijichafua na kusababisha ngozi yake ibadilike na kuwa nyeusi. Nywele zake hazikutamanika, kwa kumwangalia mara moja tu hukuhitaji ufafanuzi kugundua hali yake ya akili. 
Pamoja na hali hiyo, babu Ayubu hakukoma kumwingilia Nancy kimwili, suala la wendawazimu halikusumbua ubongo wake, alimfanyia kila aina ya ukatili akiwa kwenye kamba kama mateka, hakuyajali matatizo yake hata kidogo, kitu cha maana kwake ilikuwa kujistarehesha. 
Miezi mitatu baadaye walikuwa wangali kisiwani wakipata mateso, mama yake Nancy aliishakata tamaa ya kuokolewa na kuamini hapakuwa na njia ya wao kuondoka tena kisiwani, hayo yaliishakuwa maisha yao na waliishakubaliana nayo. 
Afya ya mtoto wake iliharibika kupita kiasi kwa sababu ya kugoma kula, mara nyingi alikuwa mgonjwa na alipoteza uzito mkubwa wa mwili wake ! Kwa sababu ya kutokuwepo kwa tiba yoyote pale kisiwani, matumaini kuwa siku moja mama Nancy angeondoka na mwanae akiwa salama yalipotea. 
Bado hapakuwa na maongezi kati yao, Nancy hakuongea kitu na mama yake ! kila alipomsogelea alilia, maneno pekee ambayo mama huyu alikumbuka kuongea na mwanae ni yale aliyosema wakati anamsimulia juu ya mateso aliyoyapata kisiwani akilazimishwa kufanya ngono, hali hiyo ilimuumiza sana mama Nancy, mara kwa mara alitamani kuongea na mtoto wake lakini haikuwezekana ! Akili yake iliishaharibika. 
“ Yote haya ni kwa sababu ya Tonny na sijui ni kwanini alimpeleka mwanangu kwa mganga kula kiapo ? ” Aliwaza mama Nancy. Mama Nancy alikuwa kama mke wa ndoa wa mzee Kiwembe, hakuyapenda maisha hayo na hakumpenda mzee huyo lakini hakuwa na chaguo jingine, alielewa wazi kuwa kumkataa kungemaanisha kifo chake na pengine cha mwanae ! Akiyafanya yote aliyotakiwa kufanya ili maisha yao yawe salama akitegemea labda siku moja wangeokolewa kutoka mikononi mwa wauaji. 
Tumbo lake halikuwa la kawaida, lilikuwa kubwa kuashiria tayari alikuwa mjamzito ! Mimba ya mzee Kiwembe, jambo hilo lilimuumiza sana, mchana na usiku alilia lakini hakuweza kuubadilisha ukweli kuwa tayari alikuwa na mimba ya mtu ambaye hakuwa na mapenzi naye hata chembe. 
Hakuwa na jibu la kumpa mume wake kama ingetokea siku moja akatoroka na kurudi nyumbani, alishindwa kuelewa ni maneno gani angesema ili mume wake amwelewe kwamba yote yaliyotokea hayakuwa mapenzi yake bali alilazimishwa ! Kwa hasira za mzee Katobe lazima angeuawa baada ya kuonekana msaliti. 
“ Mungu atanisamehe sikuwa na chaguo haya si mapenzi yangu ! Na namwomba Mungu asaidie Nancy pia asije akapewa mimba maana babu Ayubu anamwingilia kila siku bila huruma” Aliendelea kuwaza huku akitayarisha chakula jikoni huku mzee Kiwembe akiwa amejilaza kwenye jamvi walilolitumia kama kitanda. 
Afya ya mtoto wake ilizidi kumtisha alizidi kukonda kadiri siku zilivyokwenda ! Maisha yake yalikuwa hatarini, kila siku alimlilia mzee Kiwembe ili wampeleke aidha hospitali Kigoma au popote karibu lakini hakusikilizwa, alizidi kunyweshwa mizizi ya miti isiyoeleweka kila siku “ Kama Nancy atakufa, mimi pia sitakuwa na sababu ya kuendelea kuishi, nitajinyonga na kufa mara moja !” Aliwaza mama Nancy akiwa amekaa chini na kumwangalia mtoto wake aliyelala chini mikono na miguu yake ikiwa imefungwa kwenye nguzo.

Je nini kitaendelea?U YA 21
Endelea kutembelea app yetu ujue zaidi