TAFUTA HAPA

HADITHI: Damu, mabusu na machozi SEHEMU YA 19

Nancy alimwangalia baby Ayoub kwa macho ya chuki, hakuwa tayari kufanya kitendo alichokuwa akiambia hata kama angewekewa kisu shingoni, kiapo alichokula kwa mganga bado kilimsumbua kichwani mwake! Alielewa wazi kufanya tendo la ndoa na mwanaume mwingine tofauti na Tonny kabla hajakutana na mzee Mwinyimkuu na kukiondoa kiapo chake, kungemletea madhara makubwa. Alikuwa tayari kuchagua kifo lakini si kumvulia babu Ayoub nguo yake ya ndani.
“Umeielewa!”
“Wewe hivisasa ni mke wangu, siamini kama kweli nimekutana na mwanamke baada ya miaka kumi na zaidi! Ungekufa ningesikitika sana ndio maana nilikuwa najitahidi kadir ya uwezo wangu wote ili upone nami nianza kula uhondo kama mwenzangu mzee kiwembe!”
“Kama ni kuniua niue lakini kitu unachosema hakiwezi kufanyika!”
“Haya subiri usiku utaona!”
“tafadhali nionyesha mahali mama yangu alipo!” Alisema Nancy.
Babu Ayoub alimsaidia Nnacy kunyanyuka kutoka mahali alipokuwa amelala na kumwongoza hadi kwenye kibanda cha nyasi kilichojengwa jirani tu na mahali kibanda cha babu Ayoub kilipokuwa, mlango ulikuwa wazi na wote wawili waliingia ndani, macho ya Nancy yaligota kwenye mgongo wa mama aliyekuwa jikoni akipika chakula! Ingawa hakumwona usoni mgongo huo ulitosha kuonyesha kuwa mwanamke huyo alikuwa mama yake, aliruka na kumkumbatia, wote wawili wakaanguka chini na kuanza kugalagala.
“Jamani mwanangu!”
“Mama!Ni wewe?”
“Ni mimi mwanangu, siamini kama uko hai tena! Umepoteza fahamu kwa karibu wiki nzima, nilishapoteza matumaini ya wewe kupona!”
“Nimenusurika mama!”
Waliendelea kukumbatiana kwa karibu dakika kumi wakilia kwa furaha, hakuna aliyekuwa tayari kuamini walikuwa salama! Wazee wawili walisimama pembeni mwao wakiwaangalia,hawakuvaa nguo yoyote mwilini mwao zaidi ya majani yaliyowafunika sehemu ya mbele! Walitisha kwa muonekano lakini wao ndio waliookoa maisha ya Nancy na mama yake.
“Mama hapa tuko wapi?” Nancy alimuuliza mama yake walipoachiana na kuketi wakiwa wameegemea ukuta.
“Ni kisiwa kinaitwa Galu!”
“Na hawa?”Nancy aliendelea kuuliza.
“Hawa wazee ndio wametuokoa! Lakini....!” Alipofika hapo mama yake Nancy alishikwa na kigugumizi, palionekana kuwa na kitu alichoshindwa kukiongea kwa wakati huo, Nancy alihisi tatizo.
“Nini mama?”
“Tutaongea baadaye!” Mama yake alinong’ona.
Mama alimwita babu Ayoub na kuanza kutambulisha kwa Nancy akisema ni binti pekee aliyejaaliwa kuwa naye katika maisha, alimshukuru kwa kuweza kumwokoa! Wakati wakiongea mama Nancy machozi yalimtoka, alikuwa na dukuduku moyoni ambalo mwanae alitamani sana kulifahamu.
“Nimemwona! Kwa hiyo wewe sasa hivi ni mama mkwe!”Aliongea babu Ayoub akitabasamu.
Mama Nancy hakujibu kitu zaidi ya kumwaga machozi zaidi ingawa babu Ayoub pamoja na mzee mwenzake waliendelea kucheka, kwao ilikuwa ni furaha kubwa mno kupata wanawake baada ya kuishi kisiwani peke yao kwa muda mrefu bila kujamiana.
“Lakini binti huyu ni binti yangu, siwezi kukuruhusu umfanyie mambo ambayo mwenzako ananifanyia mimi! Haitawezekana!”
“Ataweza tu!”Mzee Mwingine mfupi na mwenye misuli mingi mwilini aliongea huku akicheka.
Baadaye Nancy na mama yake walipewa nafasi ya kuongea peke yao, mama alisimulia habari ya kusikitisha juu ya mateso aliyoyapata mwanae akiwa usingizini! Kuna mambo alishindwa hata kuyasema kwa sababu yalikuwa aibua kwa yeye kufungua mdogo wake na kuongea mbele ya binti yake, Nancy alielewa kwa sababu tayari alishamsikia babu Ayoub akiongea.
Nancy alimweleza mama yake kuwa asingeweza kufanya kitendo cha namna hiyo sababu ya kiapo alichokula mama yake alimuunga mkono na kuahidi kumsaidia kadri alivyoweza.
“Mama suala la msingi ni kwamba tutaondokaje hapa?”
“Hata mimi sielewi, kila siku nafikiri juu ya jambo hilo lakini ni lazima tuondoke!”
“Hakuna mtumbwi?”
“Wana mtumbwi mmoja tu mdogo na huo ndio wanaoutumia kwenda kutega samaki, sidhani kama unaweza kutufikisha ng’ambo!”
“Sasa tutafanyaje?”
“Hakuna kitu kingine zaidi ya kujifanya tumekubaliana na wanachokisema ili watuzoee na kutuamini, wakati huohuo nitakuwa najifunza kupiga kasia na kuutumia mtumbwi wao ili kama nikifanikiwa kuuelewa tutajaribu kutoroka siku moja usiku!’
“Sawa mama!Lakini kumbuka mimi sitaweza kufanya tendo la ndoa na babu Ayoub!’
“Hapo sijui tutafanya kitu gani, maana mimi pia nilikataa lakini kipigo nilichopata nilijikuta nalainika na kukubali namwomba Mungu usikutane na mateso kama niliyoyapata mimi!” Aliongea mama yake Nancy na kuzidi kumtisha.
Waliporudi ndani Nancy aliketi chini na kuendelea kumshuhudia mama yake akitayarisha chakula, hapakuwa na chakula kingine kisiwani zaidi ya samaki hivyo muda mfupi tu baadaye chakula kilikuwa tayari na wote wanne walitengeneza mduara na kuanza kula, wakati wanamaliza zoezi hilo tayari ilikuwa saa kumi na mbili ya jioni.
“Twende!”Mzee Ayoub alimwamrisha Nancy.
“Wapi?”
“Nyumbani kwetu!”
“Mimi siondoki hapa! Sitaki kutengana na mama yangu!”
“Wewe unafanya utani sio?”
“Sio utani namaanisha ninachokisema, nimekwishakueleza kwamba sipo tayari kufanya tendo la ndoa kwa sababu nilishakula kiapo lakini husikii?”
“Mzee Kiwembe hebu lete ile nahiii! Tumekupa muda wa kuongea na mama yako ina maana hajakueleza yaliyompata?”
“Kanieleza lakini siwezi ni bora kufa!”
“Haya sasa, acha tuone nani atakuwa mshindi!”Aliongea babu Ayoub baada ya kukabidhiwa fimbo nyembamba iliyokatwa kutoka kwa mnyama wa majini aitwaye Kiboko!
“Nyanyuka!”
“Sinyanyuki!”
“Chaaaaaa!Chaaaa!”Fimbo hiyo nyembamba ilipita mgongoni mwa Nancy, akalia na kujikunjakunja na nyingine zaidi zikazidi kumiminika wakati mzee Kiwembe akimfunga Nancy mguu kwa kamba.
“Mamaaa! Mamaaa, tafadhali nisaidie!”Aliendelea kulia kadri fimbo zilivyoendelea kupasua mgongo wake, mama yake aliumia moyoni na kujikuta akinyanyuka mahali alipokuwa akitaka kumvamia babu Ayoub lakini kabla hajamfikia alipigwa ngumi usoni na mzee kiwembe akaanguka chini.
hakika walikuwa katika mateso na hawakujua jinsi ya kujiokoa, akiwa amelala chini mama alishuhudia mwanae akibebwa juujuu na wazee hao wawili kupelekwa kwenye kibanda cha babu Ayoub, huko alimsikia akiendelea kulia na kuomba msaada, alitamani kumsaidia lakini hakuwa na uwezo huo, maisha aliyokuwa akiyapitia Nancy ndiyo aliyoyapitia yeye karibu kila siku mpaka alipokubali kufanywa mke wa mzee Kiwembe.
Masaa matatu baadaye mzee Kiwembe akiwa amesharejea kwenye kibanda chake na kuendelea kumfanyia mama Nancy mambo yasiyostahili, kibandani kwa babu Ayoub nako kukawa kimya!Mama Nancy alielewa walishamchosha mtoto wake kwa kipigo na kujikuta akiwa tayari kwa lolote alilotaka kufanyiwa.
“Najua anamwingilia na sijui kitakachotokea ni nini?” Alijiuliza mama Nancy akilini mwake akifikiria kiapo.

Je nini kitaendelea?
Je Nancy na mama yake wataweza kutoka ndani ya kisiwa hicho?