TAFUTA HAPA

HADITHI: Damu, mabusu na machozi SEHEMU YA PILI:



Kadri Nancy alivyozidi kukua ndivyo uzuri na maumbile yake ya nyuma yalivyozidi kuongezeka, cha kushangaza alizidi kukonda juu! Kama ungefanikiwa kuona picha yake ungefikiri ilikuwa ni picha ya kuchora au kutengenezwa kwenye kompyuta, halikuwa jambo rahisi mtu kukubali kuwa umbile lile ulikuwa mwili wake kama si matambala! Akiwa darasa la saba jina lake lilibadilika akawa anaitwa ‘Nyambizi’ akilinganishwa na meli kubwa zisafirizo chini ya maji!
Nancy alikuwa tishio si kwa sura na uzuri tu bali pia darasani mara kwa mara alishika namba moja darasani mwake hapo ndipo alipowashangaza watu, karibu wanafunzi shule nzima walimtamani lakini hawakufanikiwa kumpata, katika miaka yote saba aliyosoma shule ya msingi Mwanamakuka alishafukuzisha kazi walimu watano waliomwita ofisini na kutaka kumbaka! Huyo ndiyo alikuwa Nancy Nyambizi.
Alielewana na kijana mmoja tu shuleni kwao, huyo ndiye waliyegombania naye namba darasani, aliitwa Antony Kivembe au Tony! Alikuwa mtoto wa mama mjane mwenye shida pengine kuliko wajane wote wilayani Bagamoyo, alijulikana na watu wengi kwa jina la mama Tony ingawa jina lake halisi aliitwa Irene Ngowika. Mama huyu naye hakuwa na mtoto mwingine zaidi ya Tony! Umaskini uliigubika familia yake, ni mwanae ndiye aliyekwenda nyumban kwao na Nancy kufuata kitabu chake cha Kiswahili na kukamatwa na mzee Katobe kisha kuingizwa ndani na kuumishwa mbwa.
Nancy alikerwa sana na kitendo hicho, alijifungia ndani na kulia usiku mzima, hakutaka kabisa rafiki yake mpendwa afanyiwe kitu kibaya, alimtegemea Tony sana katika mambo mengi ya masomo kwani alikuwa tofauti na wavulana wengine shuleni, hata siku moja hakuwakuwahi kumtamkia kitu chochote kuhusiana na mapenzi! Siku iliyofuata Nancy aliongea na baba yake na kumweleza ubaya wa kitendo alichokifanya tena akilia machozi.
“Huyo ndiye hunisaidia mimi katika masomo yangu shuleni! Kwanini umemfanyia hivyo?”
“Sikufahamu jambo hilo mwanangu, nisamehe!” alijibu mzee Katobe na siku iliyofuata ilibidi dereva atumwe kwenda hadi nyumbani kwao na Tony na kumchukua kisha kumpeleka hospitali ambako alitibiwa na kuweza kuchomwa sindano za chanjo ya kichaa cha mbwa, wiki mbili baadae alikuwa salama salimini na yeye na mama yake walikaribishwa nyumbani kwa mzee Katobe kwa chakula cha jioni kuimarisha zaidi uhusiano wao na tangu siku hiyo mzee Katobe alimruhusu Tony kumtembelea Nancy nyumbani na hata kusoma pamoja.
“Nisamehe sana Tony! Ni makosa ya baba nipo tayari kuyabeba!” Nancy alimwambia Tony.
“Hamna shida wewe ni dada yangu Nancy, siwezi kumchukia baba yako, kwani hata mimi namchukulia kama baba yangu, nimekwishamsamehe!”
“Nashukuru sana kwa hilo!”
Ukaribu wao uliongezeka maradufu baada ya hapo, mara kwa mara Tony akawa anakwenda nyumbani kwao na Nancy kujisomea nyakati za usiku, walisoma hadi katikati ya usiku bila mzee Katobe na mke wake kuwa na wasiwasi, walimwamini Tony kuliko hata walivyomwamini binti yao Nancy. Usiku walipochoka Tony alilala chumba cha wageni na Nancy alikwenda chumbani kwake na asubuhi waliondoka pamoja kwenda shuleni!
“Nancy acha!” Tony alisema kwa sauti ya chini, ilikuwa ni tayari saa saba ya usiku, Nancy alikuwa akimvuta ili ampige busu mdomoni, mwili wake ulikuwa ulikuwa ukihisi kitu kisicho cha kawaida ambacho hakuwahi kupambana nacho maishani, zilikuwa ni hisia za mapenzi zilizosambaa mwili mzima.
“Niache nini Tony? Mimi nakupenda sana, kila binadamu hapa duniani anahitaji kuwa na mpenzi, kwani wewe hufahamu wimbo wa Chaka Chaka usemao Every woman needs love?”
“Hata kama naufahamu haifai sisi kufanya kitu unachotaka tufanye, sisi bado wadogo sana Nancy, inabidi tusubiri kwanza!”
“Haiwezekani kusubiri!” Alisema Nancy na kumwangukia Tony kifuani na wote wakaanguka sakafuni, katika kufanya hivyo bahati mbaya alikigonga kiti kimoja kikaanguka chini na kusababisha kelele zilizokwenda hadi chumbani kwa baba yake, Nancy hakujali akiamini mzee Katobe alikuwa usingizini na kwa haraka alivua gauni lake na kumlalia Tony kifuani!
“Njoo! Njoo! Njoo Tony, usipokubali kufanya ninachotaka nitamwambia baba yangu kuwa ulitaka kunibaka!”
Kauli hiyo ilifanya mwili wote wa Tony utetemeke, alimwogopa mzee Katobe kuliko kitu kingine chochote ukimwondoa Mungu! Alijua kama Nancy angefungua mdomo wake na kusema maneno hayo, Tony angeuawa kwa risasi. Huku akitetemeka alimwomba Nancy atoke kwanza kifuani ili avue kaptula yake haraka na amtimizie haja yake, kweli Nancy alifanya hivyo na Tony akasimama wima na kufungua vifungo vyote vya kaptula yake na kuteremsha pamoja na nguo yake ya ndani akabaki kama alivyozaliwa.
“Njoo upesi mwisho baba atakuja!”
“Sijui, sijawahi kufanya!”
“Wewe njoo tu nitakuonyesha!”
Huku akitetemeka Tony alianguka juu ya mwili wa Nancy tayari kwa kufanya alilotakiwa kutenda, alishasahau kuwa ni dhambi! Ghafla akiwa juu ya mwili wa Nancy mlango wa chumbani kwa mzee Katobe ukifunguliwa na mzee Katobe akatokeza na kusimama wima, Tony alihisi haja kubwa na ndogo ikipenya bila amri yake!
“Unaona sasa?”
“Nini?”
“Mzee Katobe!”
“Yuko wapi?”
“Yule pale mlangoni!” Alijibu Tony akitetemeka mwili mzima kwa hofu, alielewa ambacho kingetokea kama mzee Katobe angemshuhudia akiwa juu ya kifua cha mtoto wake aliyempenda kuliko kitu chochote duniani, ni wazi kifo kingekuwa halali yake, alizidi kutetemeka akiwa amepigwa ganzi bila kujua la kufanya, alimshudia mzee Katobe akitembea kutoka sehemu moja ya chumba kwenda nyingine huku akisonya!
Tony alibana pumzi yake, hakutaka isikike na taratibu aliporomoka toka kifuani kwa Nancy na kuingia chini ya meza Nancy akimfuata nyuma, hata yeye alikuwa na hofu! Alimuelewa baba yake kwa kina, ingawa asingeuawa kama mwenzake Tony adhabu ambayo angeipata lazima angeisimulia maishani mwake, wakiwa chini ya kiti walimshuhudia mzee Katobe akipita taratibu na kuzima taa iliyokuwepo sebuleni.
“Hawa watoto bwana hawajui hata gharama ya umeme zilivyokubwa , wanaacha taa zinawaka ovyo!” Alisema mzee Katobe baada ya kuzima taa na kunyoosha moja kwa moja hadi ulipokuwa mlango wa kuingia chumbani kwake, akausukuma na kuingia ndani.
Tony alishusha pumzi kwa nguvu akiwa chini ya meza, hakuamini kama alikuwa amenusurika na kifo! Hazikuwa juhudi zake bali mpango wa Mungu kumuondolea mzee Katobe wazo la kuangalia chini ya meza, rohoni mwake aliapa kutorudia tena tendo hilo kwani lilikuwa ni hatari kwa maisha yake, akiwaza hilo ghafla alishtukia akiguswa ubavuni.
“Tony!”
“Unasemaje?”
“Tunaendelea!”
“Nanini?”
“Unajifanya kuuliza, ina maana umesahau tulikuwa na programu gani kabla ya mzee Katobe hajatokeza toka chumbani?”
“Nakumbuka lakini hilo si jambo jema Nancy, wewe ni kama dada yangu!”
“Wewe ndio unaelewa hayo, mimi nataka tucheze tu na kama hutaki swala ni lile lile kuwa nitapiga kelele nimtaarifu baba kwamba unataka kunibaka!”
“Nancy bado una wazo hilo?”
“Ndio kama tu hutakubali kufanya ninachotaka! Hutaki?”
Tony alinyanyuka na kukaa kitako kisha kuinamisha kichwa chake chini akiwaza,alikuwa katika wakati mgumu wa kuchagua maisha au kutenda alichotakiwa kufanya, kwa sababu alipenda kuendelea na maisha, bila kutaka Tony alijikuta akihiari kufanya tendo la ndoa na Nancy, alipovutwa alisogea karibu na alipoamliwa kupanda juu alifanya hivyo kwa kutetemeka. Ilikuwa mara ya kwanza maishani kwake kutakiwa kutimiza wajibu mgumu kama huo, siku zote alilitafsiri tendo la ndoa kama jambo lililotakiwa kusubiri mpaka watu waoane.
Wote wawili walikuwa wageni wa jambo hilo, hata Nancy pia hakuwahi kukutana na mwanaume maishani mwake, ni maneno ya wanafunzi wenzake shuleni ndio yaliyomsisimua na kumfanya ajikute akitamani kujaribu na mtu pekee wa kufanya naye majaribio alikuwa Tony! Mvulana aliyeishi naye ndani ya nyumba yao ambaye baba yake asingeweza kumfikiria vibaya. Kwa sababu ya ugeni na tendo hilo hakuna walilolifanya wakiwa sakafuni zaidi ya kupapasana na kufanya mambo ambayo waliyaona katika mchezo wa Egoli, kwao hiyo ilitosha kwani walipoachia nusu saa baadaye jasho lilikuwa likiwatoka na kila mmoja akanyanyuka na kuelekea chumbani kwake, walikuwa wameridhika.
Wakati chumbani Nancy alifurahia kilichotokea, Tony alikuwa akilia machozi, alifanya kitendo ambacho hakukipenda lakini hakuwa na la kufanya zaidi ya kukubali, asubuhi kulipokucha alikuwa mnyonge kupita kiasi, alijisikia mkosaji ndani ya moyo wake hata alipomwamkia mzee Katobe.
“Mbona unaonekana mnyonge leo?” Mzee Katobe aliuliza.
“Ninaumwa”
“Unaumwa nini?”
“Naumwa kichwa!”
“Pole, utaweza kwenda shuleni?”
“Nitaweza baba!”
“Ok, baadae tutaonana!”
Shuleni Tony hakuongea kitu na Nancy, alionyesha wazi kuchukizwa na kitendo kilichofanyika usiku na katika maongezi yao hakuficha kilichokuwa moyoni mwake, wakati wanaondoka shule hakutaka kuongozana na Nancy tabia yake ya siku hiyo hata wanafunzi wenzake waliitilia mashaka, wengi walihisi kulikuwa na ugomvi kati yao! Aliondoka shuleni peke yake tena mapema kabla ya wanafunzi wengine hawajaruhusiwa, badala ya kurudi nyumbani kwa mzee Katobe alinyoosha moja kwa moja kwenda nyumbani kwa mama yake eneo la Magomeni mjini Bagamoyo kama kilometa kumi kutoka shuleni kwao.
Alimkuta mama yake akiendelea na shughuli za nyumbani kama kawaida, hata yeye pia hali ya mwanae ilimshangaza akajikuta akilazimika kumkarisha Tony chini ili aeleze kilichokuwa kikimsumbua! Hakuwa na kitu cha kumwambia mama yake, kamwe asingeweza kufungua mdomo wake na kusema kwa mama yake alifanya tendo la ndoa wakati alielewa siku zote alikemea kitendo hicho na alikiita ni dhambi kubwa sana mpaka pale kilipohalalishwa kanisani.
“Nieleze nini kinakusumbua mwanangu?”
“Hakuna kitu chochote!”
“Wewe ni mwanangu Tony, nilikuzaa mimi, tabia yako lazima niielewe kuna kitu kinakusumbua Tony!”
“Hakuna kitu mama ila nataka tu kukueleza kwamba sitarudi tena nyumbani kwa mzee Katobe!”
“We mtoto! Umefanya nini tena? Kwa nini hutaki kurudi? Nani atakulipia ada ya shule? Huelewi kuwa mzee Katobe ameamua kukusomesha mpaka sekondari na hata Chuo Kikuu?”
“Pamoja na hayo yote mama, sipo tayari kurudi tena nyumbani kwa mzee Katobe!”
“Lakini kwanini?”
“Maisha yangu ni kitu cha muhimu sana mama!”
“Unamaanisha nini Tony?”
“Kurudi kwa mzee Katobe itakuwa ni sawa na kuuza uhai wangu, iko siku nitarudishwa hapa nikiwa maiti wakati wewe ni mama yangu na mimi ni mtoto wako pekee! Hunipendi mama?”
“Nakupenda mwanangu!”
“Basi niache niishi na wewe kama tulivyokuwa tukiishi zamani!”
“Hata hivyo nahitaji kufahamu kilichotokea!”
Je nini kitaendelea?