TAFUTA HAPA

HADITHI: Damu, mabusu na machozi sehemu ya 1

MWANZONI


Kwa muda mrefu sana mvua ilikuwa haijanyesha katika wilaya ya Bagamoyo, mkoa wa Pwani mazao ya watu wengi sana yalikuwa yamekufa mashambani, kulikuwa na dalili zote za kutokea kwa balaa la njaa! Jambo hili lilisababisha watu wengi kuwa na wasiwasi ni wapi wangepata chakula.
Pamoja na hali hiyo ya wasiwasi, siku hiyo ya Ijumaa baada ya swala ya Ijumaa Kuu wazee wote walikusanyika chini ya mti mkubwa wa mwembe uliopo katika eneo la Kajificheni kulikuwa na mkutano wa hadhara ulioitishwa na mwenyekiti wa mtaa wa Kajificheni! Mkutano huu haukuitishwa kuongelea tishio la njaa lililokuwa likitegemewa! Bali wakazi wa Bagamoyo walitaka kumjadili mtu mmoja hatari katika wilaya yao, huyo hakuwa mwingine bali mzee Wilbord Katobe, mfanyabiashara aliyemiliki vyombo mbalimbali vya uvuvi majini na alikuwa na kiwanda cha kusindika samaki aina ya Kamba na pia alimiliki mashamba makubwa ya nazi na mananasi maeneo ya Kiwangwa huko huko Bagamoyo. Kifupi alikuwa mfanyabiashara tajiri kwa ngazi ya wilaya ya Bagamoyo.
Ulikuwa ni mkutano kumjadili mzee huyu aliyesifika kwa ukorofi wake, hasa lilipokuja suala la mtoto wake mmoja wa kike! Alishawajeruhi vijana wapatao watatu kwa risasi na mapanga sababu ya binti yake, eti walimtaka mapenzi. Wakazi wa Bagamoyo hawakupenda kabisa vitendo hivyo na siku hiyo ndio ulikuwa mkutano wa kumjadili, wazee walitaka kumuongelea na ikabidi wapeleke mapendekezo yao mkoani baada ya kuona serikali ya wilaya imeshindwa kabisa kumshughulikia, mara kadhaa walisharipoti suala hilo polisi lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake!
Wananchi walikuwa wamechoka, siku moja kabla ya mkutano huo mzee Katobe alimkamata kijana mmoja aliyesoma Shule ya Msingi Mwanamakuka pamoja na binti yake, alifika nyumbani hapo kufuata kitabu chake cha Kiswahili alichomwazimisha binti wa mzee Katobe ambaye alifikiri kijana huyo alikuja nyumbani kwake kumtaka mtoto wake kimapenzi.
Alimkamata na kumvutia ndani ya ngome ya nyumba yake kisha kuwaachia mbwa wake kumi na mbili ili wamshambulie, kazi hiyo ilifanyika kikamilifu kijana alipoachiwa nusu saa baadae mwili wake wote ulijaa majeraha ya kuumwa na mbwa, majeraha yake yalivuja damu nyingi mfululizo! Kitendo hicho kiliwakera sana wazee wa mji wa Bagamoyo ndio sababu waliamua kuitisha kikao cha kumjadili mzee Katobe!
“Haiwezekani, kwani yeye ni nani? Yeye ndiye ana binti peke yake hapa mjini?”
“Hana nidhamu kabisa mzee huyu, anamchunga mtoto wake kwani yeye ndiye atamwoa?”
“Aondoke Bagamoyo!”
“Tutamchukua tu binti yake, hata akimlinda vipi? Huyo ni msichana wetu tu!”
Watu walizidi kupiga kelele kwenye mkutano huo wakimsubiri mzee Katobe aliyepelekewa taarifa za kikao hicho afike, hata hivyo hakufika na kikao kwa sababu alikidharau, kikawa kimefungwa masaa mawili baadae wazazi wote wakiwa wameazimia kupambana nae kama polisi isingeingilia kati, walidai tabia ya kuwatesa watoto wao ilikuwa imewachosha!
“Tutapambana nae!” Aliongea mmoja wa wazee.
“Hakyanani siku atakayoniingiza mimi ndani ya nyumba yake kuniumisha mbwa nitamng’ang’ania mpaka nife nae, haiwezekani, hapa kijijini mbona wapo wazee wengi tu wenye mabinti kwanini hawafanyi hivi, huyu mzee mwendawazimu! We acha tu, ipo siku yake!” Kijana mmoja alilalama.
Mzee Katobe alitisha, alikuwa mzee katili ambaye hakujali maoni ya watu juu yake, hakujali walimpenda au la! Ukatili wake ulijulikana mkoa nzima wa pwani na hata mkoa wa Dar es Salaam, hakuwa mtu wa kugusika kirahisi wengine walihisi alikuwa na mkono ndani ya Serikali kwa sababu alikuwa na uwezo wa kupindisha sheria pale alipotaka kufanya hivyo na hakuna lililofanyika! Ujeuri wake ulikuwa tishio hata baadhi ya viongozi wa wilaya na mkoa.
Pamoja na kuishi na mke wake kwa miaka zaidi ya ishirini mzee Katobe alifanikiwa kuzaa mtoto mmoja tu, tena wa kike binti huyu aliitwa Nancy! Alikuwa kipenzi kikubwa cha baba yake, mzee Katobe alikuwa tayari kutumia chochote alichokuwa nacho ili mtoto wake pekee apate elimu bora ambayo ingemwezesha kuziendesha vizuri mali zake mara atakapostaafu kazi kwa sababu ya uzee au kitu chochote.
“Tulia mwanangu Nancy, wewe ni msichana mzuri na mimi baba yako nina kila kitu hapa nyumbani, usibabaishwe na hawa vijana wa Bagamoyo hawana lolote, wavuvi tu! Watakupa kitu gani hawa? Soma mwanangu, mali yote niliyokuwa nayo mimi ni yako kama hutapata elimu ya kutosha utashindwa kuendesha kazi zangu kesho na keshokutwa mimi na mama yako tukiondoka!” Mzee Katobe alimhusia binti yake.
“Sawa baba nitajitahidi kufanya yote yatakayokufurahisha wewe mzazi wangu!”
“Ukimaliza tu darasa la saba, nitakupeleka Uingereza ukasome masomo ya sekondari na hata chuo kikuu, sitaki ukae hapa Bagamoyo!”
“Sawa baba!” Aliitikia Nancy kwa unyenyekevu mbele ya baba yake, aliamini baba yake alikuwa tajiri kuliko mtu yeyote Bagamoyo, hilo lilimpa majivuno na hali ya kujiamini kupita kiasi.
Wakati baba yake alitisha kwa ukali na ukorofi binti alitisha kwa uzuri wa sura na mvuto, katika umri wa maiaka kumi na mbili tu Nancy alikuwa tishio wilayani Bagamoyo na mkoa wa Pwani kwa ujumla, sifa zake zilisambaa kama upepo! Umbile lake lilitisha, alikuwa na makalio makubwa yasiyo na maelezo ya kutosheleza, alirithi hali hiyo kutoka kwa mama yake Ashura Mwinyimkuu, mwanamke mwenye mchanganyiko wa Mkwere na Mnyarwanda.
Nancy alikuwa na mwili mkubwa uliomfanya aonekane kama binti mwenye umri wa maiak 18 au zaidi na alikuwa na ngozi nyororo yenye rangi ya chokleti! Meno yake yalipangika kisawasawa mdomoni! Alikuwa mwembamba juu lakini mkubwa chini, hii ilimaanisha hata miguu yake pia ilikiwa fiti! Alivutia kumwangalia kwa macho na kushangaa uumbaji wa Mungu, mama yake alikuwa mfupi lakini baba yake alikuwa mrefu na ni kitu hicho ndicho pekee ambacho Nancy alichorithi kutoka kwa baba yake mzee Katobe.
Mtu yeyote aliyefungua mdomo wake na kusema Nancy alikuwa mzuri hakukosea ni kweli msichana huyo mdogo alivutia, vijana wengi mjini Bagamoyo hata wengine kutoka jijini Dar es Salaam walishajaribu kumfuata wakimtaka kimapenzi lakini hawakufanikiwa, waliishia kupambana na mzee Katobe na kupigwa hata kujeruhiwa kwa mapanga na kukoswakoswa kwa risasi.
Mzee Katobe alimchunga binti yake kuliko askari alivyomchunga mtuhumiwa wa mauaji! Mambo haya yaliwafanya vijana wengi mjini Bagamoyo wamwogope binti huyo! Waliogopa kufa, maana kuna wakati mzee Katobe aliwahi kutoa vitisho vya kumloga kijana yeyote ambaye angeendelea kumsumbua binti yake kipenzi, Nancy.
“Aisee huyu mtoto ni mkali?” Mmoja wa vijana alisema.
“Arooo, cheki! Cheki! Mtoto kajazia idara zote, kaenda juu sekunde mtoto! Aisee huyo anakuja!
“Wewe, kirusi umeweka katika hiyo listi?”
“Ebwanae usilete mambo ya matangazo ya Ukimwi hapa, angalia toto liko fiti ….!” Aliendelea kusema kijana mwingine, wote wawili walikuwa wamesimama kwenye njia ya kutoka shule ya msingi Mwanamakuka wakisubiri wanafunzi watoke shuleni, Nancy alikuwa anapita mbele yao akiongozana na kijana mmoja mweusi aliyefunga bandeji usoni na mikononi kama aliyejeruhiwa.
“Ebwana mie namtokea!”
“Baba yake unamfahamu lakini? Isitoshe utamtokeaje mtu unayemwona ana boyifrend wake?”
“Ni mtoto wa nani? Huyo ndiye boyifrendi wake?”
“Mzee Katobe! Huyo kijana anaitwa Tony sidhani kama ni boyifrendi wake ila mara kwa mara huwa wanaonekana wote”
“Hivi huyu ndiye Nancy?”
“Ndiye!”
“Aisee hapo sitii mguu! Baba yake nuksi ile mbaya, lakini muone anavyotingishika huko nyuma! Ebwanae! Namsifia Mungu kwa uumbaji! Mungu anajua kuchora ramani, lakini ana upendeleo ramani ya huyu binti ni ya uhakika tena selfu kontena, siyo ramani kama yako kibakuli, utafikiri mkate!” Kijana alimtania mwenzake akicheka.
“Ebwanae mimi utani unaoelekea kwenye ukweli huwa sitaki, Ngovongo ukirudia tena tutagombana!”
“Samahani mshkaji, nilikuwa naweka msisitizo juu ya ramani za Mungu, sikutegemea ungemaindi.”
Je nini kitaendelea?