JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 5
INAENDELEA HAPA:
Baada ya kuvutana sana kati ya Mwalimu mkuu na Mr.  Brown ofisini ikabidi mwalimu mkuu akubali kuwa mpole na kurudisha pesa  japo sio zote ilibidi mwalimu mkuu atoe nusu ya pesa zilizolipwa, Mr.  Brown alilipa ada Shilingi laki moja na nusu ikabidi mwalimu mkuu atoe  nusu ya pesa hizi Shilingi elfu sabini na tano na kumpa Mr. Brown. Mr.  Brown akapokea zile pesa Shilingi elfu Sabini na tano akamchukua binti  yake JENIFER wakaondoka na kuelekea nyumbani kipindi wapo njiani  wanaelekea nyumbani, Mr. Brown alikua na hasira sana akamwambia binti  yake JENIFER "We mtoto leo tukifika tu nyumbani chukua nguo zako na  uondoke nyumbani kwangu sitaki kukuona, mshenzi wewe!". Walipofika  nyumbani tu Mr. Brown akaanza kumuhadithia mke wake Mrs. Brown  yaliyotokea shuleni kuhusu binti yao JENIFER na akamwambia Mrs. Brown  kuwa hataki hata kumuona aondoke nyumbani kwake lakini kwa maamuzi haya  ya Mr. Brown mke wake Mrs. Brown hakuafikiana nayo akamwambia mume wake
"SASA MUME WANGU UNAMFUKUZA MTOTO AENDE WAPI WAKATI  HAPA NDIO KWAO, UNADHANI ATAENDA WAPI? KAMA MAJI YAMEISHAMWAGIKA MAKOSA  NDIO KISHAFANYA HAKUNA JINSI NI KUMSAMEHE NA TUKAE TUSHAURIANE TUJUE  TUNAFANYAJE MUME WANGU PUNGUZA HASIRA". Mr. Brown akamjibu "HAIWEZEKANI  MIMI SITAKI HATA KUMUONA HUMU NDANI AONDOKE SITAKI KUMUONA". Mrs. Brown  nae akamjibu "KAMA UNATAKA HUYU BINTI AONDOKE HUMU NDANI BASI JUA  NITAONDOKA NAE SIWEZI KUKUBALI BINTI YANGU AONDOKE AKAPATE SHIDA WAKATI  KWAO ANAPO, UKIMFUKUZA JUA NAMIMI NAONDOKA HUMU NDANI" Baada ya Mrs.  Brown kumuambia Mume wake Mr. Brown maneno hayo ghafla Mr. Brown alisema  kwa sauti kali ya juu "SAWA MKITAKA MUONDOKE WOTE, SIWEZI KUFUGA  UPUMBAVU KAMA UNAONA NAMUONEA MTOTO WAKO MFUATE MUONDOKE WOTE PUMBAVU!".  Mrs Brown akamjibu "EH E! TAFADHALI BABA WEE, USINITUKANE NGOJA  TUKUPISHE UBAKIE NA NYUMBA YAKO SIO UNIFOKEE. MPUMBAVU MWENYEWE!. Ghafla  Mr. Brown alikurupuka na kumvamia mke wake Mrs. Brown na kuanza kumpiga  makofi huku akimwambia
"YANI WEWE UNADIRIKI KUNIAMBIA MIMI MPUMBAVU, WAKATI  JENIFER KAFANYA MAKOSA DHAHIRI. HIVI MIMI NINAVYOHANGAIKA KUTAFUTA PESA  ZA KUMSOMESHA HALAFU ANALETA UPUMBAVU UNAFURAHIA ETI EEH!"