JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 4
INAENDELEA HAPA:Mwalimu KABAVAKO aliwachapa kila mmoja fimbo nne  nne, kisha akawarudisha ofisini kwa mwalimu mkuu walipofika ofisini kwa  mwalimu mkuu, mwalimu mkuu aliwaambia inabidi awape adhabu ya kukaa  nyumbani mpaka uongozi wa shule utakapo kaa kikao na kuwafikiria na  kujadili kosa lao ndio wafanye maamuzi ya kuwasamehe au kutowasamehe.  Mr. Brown baba yake na JENIFER alijitahidi sana kumbembeleza mwalimu  mkuu awasamehe ili waendelee na masomo lakini mwalimu mkuu alikataa katu  katu na akamwambia Mr. Brown kuwa "MZEE KOSA WALILOFANYA HAWA WATOTO NI  KUBWA SANA TENA AFADHALI YA HAWA WENGINE KULIKO HUYU BINTI YAKO  JENIFER, JENIFER KWANZA HANA HESHIMA KADIRIKI KUMSINGIZIA MWALIMU WANGU  KUWA KAMTONGOZA WAKATI SIO KWELI HUONI KAMA HUYU MTOTO ANAWEZA KUJA  KUTUCHAFULIA SIFA YA SHULE YETU? NI BORA NIWASAMEHE HAWA WOTE LAKINI KWA  BINTI YAKO JENIFER SIWEZI KUMSAMEHE" ghafla mwalimu mkuu akabadilisha  mawazo pale pale akawaambia wale rafiki zake na JENIFER "NYIE  NIMEWASAMEHE NENDENI NYUMBANI MKAVAE NGUO ZA SHULE NA MJE DARASANI  MUENDELEE NA MASOMO ILA JENIFER SINTOWEZA KUMSAMEHE SAWA?!" wale  wanafunzi watatu ambao ni rafiki zake JENIFER walifurah na hawakuamini  kama wamesamehewa wakamshukuru sana mwalimu mkuu na wakamuahidi kuwa  hawatorudia tena, wakaondoka ofisini na kuelekea majumbani kwao kuvaa  nguo za shule. Huku ofisini mwalimu mkuu akanyanyua simu yake ya mezani  akampigia Secretary wake na kumuamuru achapishe barua ya kumsimamisha  shule mwanafunzi wake JENIFER. Mr. Brown alijitahidi sana kumbembeleza  mwalimu mkuu amsamehe binti yake mpaka machozi yakawa yanamtoka Mwalimu  mkuu akamwambia Mr. Brown "MZEE HILI NATOA FUNDISHO ILI BINTI YAKO  AJIFUNZE SIWEZI KUMSAMEHE MTOTO MSHENZI SANA HUYU" Mr. Brown  alimbembeleza sana mwalimu mkuu lakini mwalimu mkuu alimkatalia katu  katu kumsamehe JENIFER na akawaomba Mr. Brown na Binti yake JENIFER  watoke nje ya Ofisi wasubirie barua ya kusimamishwa shule binti yao.  Baada ya muda Secretary alimaliza kuchapa barua na kuipeleka ofisini kwa  mwalimu mkuu, mwalimu mkuu akamwita kiranja mkuu wa shule akamwambia  aende kupiga kengere ya dharura ili wanafunzi wote wakusanyike mstarini  aitoe barua ile hadharani mbele za wanafunzi. Kengere ilipigwa wanafunzi  wote wakatoka madarasani na kuelekea mstarini wakakusanyika wanafunzi  wote na walimu wote wa shule hiyo, mwalimu mkuu akaanza kuelezea yote  yaliyojiri kwa JENIFER na kuwajulisha wanafunzi kuwa kasimamishwa shule  baada ya hapo wakateuliwa walimu watatu wamchape fimbo JENIFER kila  mwalimu amchape fimbo tatu, kisha wanafunzi wakaruhusiwa waende  madarasani kuendelea na masomo yao. Mr. Brown alijisikia aibu sana kwani  binti yake JENIFER alichofanya ni kitu cha ajabu hivyo alikua na hasira  sana kilichomuumiza ni Ada aliyoitoa shuleni hapo ya kumlipia binti  yake akifikiria jinsi alivyoipata pesa katika mazingira magumu ilimradi  binti yake asome lakini JENIFER yote hakujali, sasa kivumbi kikaanza kwa  Mr. Brown na Mwalimu mkuu, Mr. Brown akaanza kudai pesa ya ada ya mwaka  aliyolipa shule akataka arudishiwe pesa yake ukaanza mzozo ofisini kati  ya Mwalimu mkuu na Mr. Brown hatimae wakaanza kushikana mashati  ofisini, Mr. Brown anataka pesa mwalimu mkuu anasema hatoi pesa ikawa  vurumai ofisini