TAFUTA HAPA

RAHA YA MAPENZI NI KUPENDWA(SEHEMU YA 1)

Katika maisha ya upendo,Salma anakutana na kijana mmoja aitwae Hamisi.Ilikuwa ni siku ya jumatatu asubuhi na mapema,wakati jua lilikuwa linachomoza,ndani ya jiji la Mwanza.Watu walikuwa katika pirika pirika za kuelekea kwenye kutafuta riziki.Katika hali isiyo ya kawaida,Hamisi akiwa ni mfanya biashara mkubwa pale mjini Mwanza,anasimamisha gari yake pembeni mwa Barabara,baada ya kumuona msichana mrembo,akiwa anatembea kwa miguu. Hamisi akamsalimia yule msichana,dada habari yako?Yule msichana akamjibu nzuri kaka.Hamisi akamuliza yule msichana,dada naona unatembea kwa miguu,sijui unaitwa nani?msichana akamjibu,naitwa Salma,na wewe unaitwa nani?Yule kaka akamjibu,mimi naitwa Hamisi,unaelekea wapi?Salma akamjibu Hamisi,naelekea mjini.Hamisi akamwambia Salma,hata mimi naelekea mjini.panda twende.Salma akaingia kwenye gari,Hamisi akawaswha gari moto na wakaelekea mjini. Wakiwa njiani,waliweza kuongea maongezi marefu sana,kiasi kwamba walijikuta kana kwamba wanafahamiana kwa muda mrefu sana.Hamisi alitokea kumpenda sana Salma,kutokana na maumbile yake na uzuri wa Salma jinsi ,alivyoumbika. Kwa upande wa salma alionyesha upendo wa wa kumpenda Hamisi,lakini moyoni hapakuwa na upendo zaidi ya kuwa na tamaa na utajiri alionao Hamisi. Hamisi akaegesha gari lake pembeni mwa duka la nguo za kike na manukato.Wakashuka wote kwa pamoja na kuingia kwenye duka la nguo na manukato. Hamisi akamgeukia Salma,napenda ujisikie huru,chagua nguo uipendayo na manukato.pesa ya kulipa ipo usijali.(Sehemu ya pili itaendelea kesho)